Wanasiasa wapongeza ZEC mpya.

SIKU chache baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, kuteua Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), baadhi ya viongozi wa kisiasa nchini wamesema watatoa ushirikiano wa kutosha na mwenyekiti mpya wa tume hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa chama cha ADA TADEA, Juma Ali Khatib, alisema Dk. Shein ametekeleza matakwa ya kikatiba kwa kuwashirikisha viongozi wa vyama vya siasa katika uteuzi wa tume hiyo na kwamba wameridhishwa nayo.
Alisema chama chake hakina shaka na Mwenyekiti mpya wa ZEC Jaji Mkuu Mstaafu, Hamid Hamid Mahmoud kwani mbali ya uzoefu wake lakini ni mtu mwenye kutenda haki.
Alisema anaamini uzoefu alionao Mwenyekiti huyo kama atautumia, hakuna shaka nchi itakuwa kwenye amani baada ya kumalizika chaguzi.
Makamu huyo alisema chama chake, hakina wasi wasi na uongozi na tume mpya, licha ya kuwa hakuna mpizani kutoka ndani ya chama chao, lakini walioteuliwa kuunda tume hiyo wataweza kuwawakilisha vizuri.
Zanzibarleo.

Comments