
Akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo katibu Tawala Mkoa wa Mjini Magharibi Bi
Hamida Mussa Khamis hapo ofisini kwake Vuga amesema hatua hiyo
imefanyika kutokana na sababu ya sheria hiyo na miongozo ya kiutendaji
ya imeelekeza sifa za masheha na uwezo wa mammlaka za uteuzi huo.
Aidha mkuu huyo wa mkoa ameteuwa Bi Asha Ali Ali kuwa sheha
wa shehia ya Kikwajuni juu ,Bwana Gharibub Ali Kombo kuwa Sheha wa
shehia mpya ya Mwembe Madema na Nd Soud Rajab Soud kuwa Sheha wa Shehia
ya Matarumbeta ambayo ilikuwa wazi kufutia kufariki kwa sheha wa shehia
hiyo.
Pia Mkuu wa Mkoa amemteuwa Bw Hassan Masoud Ali kuwa Sheha
wa Shehia Malindi kushika nafasi ya Nd Ramadhani Haji Mussa ambae
ameomba kutenguliwa uteuzi wake kutokana na afya yake kutokua nzuri
kulingana na majukumu ya kazi hiyo nakuomba uongonzi wa mkoa nafsi hiyo
kumpatia wananchi mwengine ambapo aliteuliwa tarehe 29/03/2018.
Kazi ya Uteuzi wa masheha hao imefanyika kutokana na sababu
mbali mbali zikiwemo nafasi tupu shehia kutokuwa na sheha maradhi,kifo
na sababu nyengine za uwajibikaji ambapo uteuzi huo umeanza tarehe 27
juni 2018.
Mzee George.
kutoka ofsi ya mkuu wa mkoa mjini magharib
kutoka ofsi ya mkuu wa mkoa mjini magharib
Zanzibar24.
Comments