
Wito huo umetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja Kamishna Msaidizi Suleiman Hassan Suleiman wakati akizungumza huko Ofisini kwake Tunguu.
Amesema kuwa ajali nyingi zinazotokea zinasababishwa kwa mwendo kasi wa magari hivyo ni vyema basi madereva kuwajali abiria wao pamoja na wanaokwenda kwa miguu ili kuepushia athari zisizokua za lazima.
Kamanda suleiman amewasisitiza madereva kwenye mwezi huu mtukufu wa ramadhan na kuelekea sikukuu wawe na utaratibu au tabia ya kuendesha vyombo vyao kwa mwendo ambao hatouweza kumletea madhara na wala kumuathiri binaadamu na kuwataka kuheshimu sheria za barabarani.
Zanzibar24
Comments