
Akizungumza na waumini wa kiislam kabla
ya kuanza kwa harakati za kutoa misaada hiyo Mwenyekiti wa jumuiya hiyo
Sheikh Mohd Sleiman Taiwani amesema kuwa jumuiya imekuwa na
utaratibu wa kutoa misaada kwa muda mrefu pale tu Mwenyezi Mungu
anapowajaalia kupata chochote kwao hawana budi kuwafikiria wale
wote ambao wanamazingira ya chini kwa mijini na vijijini.
![]() |
Mwenye kiti wqa ISTIQAMA Pemba akikabidhi msaada. |
Ameeleza kuwa kwa mika ya nyuma jumuiya
hiyo ilikua ikifunga safari na kwenda kutoa misaada katika maeneo ya vijijini
na kugundua kuwa kuna watu ambao wako ndani ya mji nao pia wanahitaji kupewa
misaada.
Aidha Mwenyekiti huyo amesema ni vyema
kwa wahisani kuangalia pia vijijini katika kutoa sadaka zao
kwani wako waumini wengi amabao wanahitaji kupewa misaada licha ya
jumuiya hiyo kujitahidi katika suala hilo .
Amesema lengo la kutoa misaada hiyo
nikutekeleza amri ya Mwenyezimungu kwa kuwafanyia ihsani kwa wale wasio jiweza.
Akizungumza kwa niamba ya Naibu Mufti
Afisa Fatwa na Utafiti wa mambo ya kiislamu Pemba Sheikh Said
Ahmed Mohd amesema katika kutekeleza amri ya Mwenyezi mungu ni vyema
kwa waumini kushindana katika mambo ya kheri ikiwemo kuwasaidi wale wasi jiweza
hususan mayatima .
Comments