Matukio
ya ukatili wa Kijinsia hapa nchini umekithiri sana ambapo jumla ya
wanawake 41,000 wameripotiwa kufanyiwa vitendo vya ukatili kwa kipindi
cha mwezi January hadi Disemba 2017 ikiwemo vitendo vya ukatili kwa
watoto 13,457 kwa kipindi hicho.
Naibu
Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Faustine
Ndugulile amesema hayo wakati wa mkutano wake na vyombo vya habari
jijini Arusha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika
yatakayoadhimishwa kwa mkoa wa Arusha tarehe 13 mwezi huu badala ya
tarehe 16 kwa sababu ya Siku Kuu ya Kitaifa ya Id El Fitri.
Naibu
Waziri huyo amesema matukio ya ukatili wa kijinsia ni mengi kuliko
matukio ya ujambazi hapa nchini na yanazidi kuendelea kila kukicha.
Ameutaja
ukatili wa kijinsia kuwa wa kimwili, kingono na ukatili wa kunyanyasa
mtu kama vile masimango na kusema ili kukabiliana na ukatili kwa
wanawake na watoto serikali imeanzisha madawati ya Jinsia kwa Jeshi la
polisi kote nchini pamoja na kuanzisha namba mpya simu ya 116 ambapo mtu
yoyote ambaye amefanyiwa ukatili wa kijinsia anaweza kuitumia kupata
msaada.
Ameongeza
kuwa Wizara imeanzisha madawati ya kamati ya ulinzi na usalama kwa
watoto katika ngazi ya Mkoa hadi Wilaya wakati huo huo akiwataka
waandishi wa habari hapa nchini kuacha kutoa taarifa za watoto
waliofanyiwa ukatili hadharani.
Amesema
ni makosa kisheria na ni ukiukwaji wa maadili ya uandishi kwa kutoa
picha na taarifa za mtoto aliyefanyiwa ukatili hadharani na kuwataka
kutomtaja jina mtoto huyo wala kutaja majina ya wazazi wao kwa kuwa ni
kinyume cha haki ya mtoto.
Serikali
ya Tanzania katika kuhakikisha kuna haki ya kuishi ya mtoto
inahakikisha kila mtoto anayezaliwa hapa nchini hapotezi maisha katika
umri mdogo na hii ni kuhakikisha haki zote zinazohusiana mtoto
zinazingatiwa.
Naibu
Waziri Ndugulile amesema kuwa Serikali imeboresha huduma za afya kwa
kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo kwa asilimia 97 na pia wakina
mama wanajifungulia katika vituo vya afya na kuhakikisha watoto wote
wananyonya maziwa ya mama kwa kipindi cha miezi sita mpaka kipindi cha
miaka miwili.
Ameongeza
kuwa Tanzania ni Nchi ya 3 katika Nchi zinazoendelea na tumetambuliwa
na Shirika la Afya Duniani kwa kufikisha asilimia 97 ya chanjo ya watoto
wote nchini , aidha kuhusiana na suala la haki ya kuendelezwa Serikali
ya Tanzania inaendelea na mikakati ya kutoa Elimu bure ili watoto
wote nchini waweze kujiendeleza kielimu.
Wakati
huo huo Naibu Waziri huyo pia ameongea na Baraza la Watoto nchini na
kusema kuwa serikali inathamini haki za watoto kwa kuwa Serikali inataka
watoto wote nchini wanazaliwa katika vituo vya Afya kwani bado kuna
asilimia 40 ya watoto bado wanazaliwa nje ya vituo vya Afya.
Aidha
ameongeza kuwa serikali itahakikisha inapunguza udumavu kwa watoto kwa
kundelea kutoa lishe bora kwa watoto na pia ili kujenga mazingira mazuri
ya watoto wenye makosa kisheria Serikali imeanzisha mahakama ya watoto
ikiwemo kuboresha mahabusu ya watoto kote nchini.
Mpekuzi.
Comments