Mkuu
wa Mkoa wa Songwe, Chiku Gallawa ametoa siku 14 kwa Mkuu wa Wilaya ya
Momba, Juma Irando na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma a na
watendaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufanya uchunguzi wa
haraka kubaini iwapo kuna wafanyabiashara waliohamishia biashara zao
Zambia.
Akizungumza
jana katika mkutano na wafanyabiashara mjini Tunduma, Gallawa alisema
ameagiza viongozi hao kufanya utafiti kwa haraka kubaini kama
wafanyabiashara wa Tanzania wamehamishia biashara zao nchini humo.
Inadaiwa
kuwa wafanyabiashara wamehamishia biashara zao Zambia kutokana na
vikwazo kutoka TRA vikiwamo utitiri wa kodi tofauti na Zambia.
“Eneo
la Tunduma ni dogo kiasi ambacho inatakiwa kuchunguzwa kutambua ni kwa
nini wafanyabiashara hao wamehama kwenda kufanya biashara hizo Zambia.
“Na imani ni kuwa uchunguzi ukishafanyika tutajua ni njia gani ya kuwarudisha na wakaendelea na shughuli zao,” alisema Gallawa.
Alisema
wafanyabiasha wa Tunduma walizoea kufanya biashara bila kulipa kodi
hivyo kuwapo mabadiliko ya sasa inawezekana ikawa ni chanzo cha wao
kuhamia Zambia na kuanzisha biashara zao huko.
Meneja
wa TRA Mkoa wa Songwe, Paul Alalaze alisema malalamiko ya wafanyabiasha
yamekuwapo kwa muda mrefu yakiwamo ya viwango vya utozwaji wa kodi
vikidaiwa kuwa vikubwa tofauti na Zambia.
Alisema
kutokana na wafanyabiashara wengi wa Tanzania kuhamia Zambia
zinafanyika jitihada za kuwaelimisha waendelee kufanya shughuli zao
nchini mwao.
“Tunawaelimisha
kuwa wanatakiwa warudi kufanyia shughuli zao Tanzania ili kuendelea
kujenga uchumi wa nchi yao na si kukimbilia Zambia ambako si kwao kwa
sababu wananufaisha watu wengine,” alisema Alalaze.
Baadhi ya wafanyabiashara walisema idadi ya wenzano wanaohamishia miradi yao Zambia inazidi kuongezeka.
Wameitaka Serikali kufanya uchunguzi kubaini ukweli wa malalamiko hayo ili kupata ufumbuzi wa kudumu.
Mpekuzi.
Comments