
Akizungumza katika uzinduzi wa mashine
mpya ya utengenezaji wa mbolea ya vidonge (UDP) iliyotengenezwa nchini
Bangaladeshi na kutolewa msaada na serikali ya watu wa Marekani I
(USAID) Waziri wa kilimo,maliasili mifugo na uvuvi Rashid Ali Juma
amesema wakulima wa mpunga wanatakiwa kutumia mbolea ya kisasa ya
vidonge ambayo itasaidia kuongeza mavuno ya mpunga kwa asilimia 30
kama tafiti zilivyoonesha.
Amesema utumiaji wa mbolea hiyo mpya ya
vidonge (UDP) kusaidia kupunguza uharibifu wa mazingira kwani kiasi
kidogo cha mbolea kinachoweza kuathiri kwenye mikondo na hali ya
hewa.
Pia amesema mbolea ya vidonge imekuja
kupunguza matumizi na gharama za uzalishaji wa mpunga ambapo mkulima
hapo awali alikuwa akitumia mifuko 3 ya UREA (MBOLEA) kwa ekari ila kwa
sasa mkulima atatumia mfuko mmoja wa mbolea ya vidonge (UDP) kwa ekari
mmoja.
Amesema uwepo wa mbolea ya vidonge
ambayo inalengo la kuongeza uzalishaji wa mpunga nchini
utaenda sambamba na sera ya wizara ya kilimo ya kuwawezesha
wakulima kuongeza uzalishaji na kulima kilimo cha biashara nchini na
kuachana na kilimo cha mazoea.
Awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi
Mkurugenzi wa kampuni ya ZAIDI Ambayo inasambaza mbegu, mbolea na dawa
zenye ubora kwa wakulima Abdullah Mohammed amesema “
tunaamini kuwa kwa mbolea ya vidonge UDP itasaidia kukuza uzalishaji na
kupelekea kujitosheleza kwa mahitaji ya chakula na kuwaongezea
wakulima kipato hali ambayo itapunguza umasikini nchini’.
Aidha amesema ZAID imekubaliana
kushirikiana na wizara ya kilimo kwa lengo la kukuza sekta ya kilimo na
kuleta mabadiliko katika kilimo cha kujikimu mtu mmoja mmoja na kuwa
kilimo cha biashara ambapo hilo litawezekana kwa kuzingatia mbinu bora
za uzalishaji na utumiaji mbegu , mbolea na dawa zenye ubora.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa mradi wa NAFAKA
James Flock amesema NAFAKA kwa kushirikiana na kampuni ya ZARI-ZAIDI
imefanikiwa kuleta technologia mpya ya uzalishaji wa mbolea ya vidonge
ya UDP hapa Zanzibar ambapo techologia hii ya pekee na ya kwanza Afrika
mashariki yenye uwezo wa kuzalisha wastani wa tani 3 za mbolea ya
vidonge kwa siku.
Aidha amesema mashine hiyo ina uwezo wa
kuzalisha mbolea takribani tani 1,000 kwa mwaka ambazo zinatosheleza
mahitaji ya wakulima wa mpunga na mboga mboga wa Zanzibar kwa asilimia
70 na mbolea itakayo zalishwa kusambazwa Unguja na Pemba kwa ajili ya
wakulima.
Nae Mkulima wa mpunga katika bonde la
Kizimbani Shafii Kibwana amesema uwepo wa mashine ya mbolea hiyo ya
vidonge umekuja kurahisisha kilimo cha mpunga nchini ambapo wao
wakulima watatumia gharama ndogo na kuzalisha mpunga kwa wingi.
Pia ameiomba serikali kuwapatiwa mbolea kwa
bei nafuu ambapo kila mkulima aweze kuimudu mbegu hiyo mpya yenye
manufaa makubwa kwa wakulima wa mpunga na mboga mboga nchini.
Uzinduzi wa mashine ya utengenezaji wa
mbolea ya vidonge UDP umefanyika Kombeni wilaya ya magharib B Unguja
na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali pamoja na wakulima wa mpunga wa
maeneo tofauti Zanzibar.
Zanzibar24.
Comments