Wizara ya elimu Zanzibar yakanusha madai ya wanasiasa.

Image result for wizara ya elimu na mafunzo ya amali zanzibarWizara ya elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar imekanusha taarifa zilizo sambazwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya kisiasa yakuwa wizara hiyo imeajiri walimu nane pekee kwa Pemba na wote kupelekwa katika skuli ya chokochoko.

Akikanusha madai hayo Afisa mdhamin  Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali  Zanzibar Mh. Salum Kitwana Sururu amesema kauli hiyo sio sahihi nakwambwa katika kipindi cha meizi mitatu iliyopita Wizaraya hiyo imeweza kutoa ajira kwa walimu wapatao 248 ndani ya Wilaya zote za Pemba kwa lengo la kuondokana uhaba wa walimu maskulini.

Akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwakwe chake chake Mh. Sururu amesema  katika kuongeza jitihada za kuleta walimu skuli ambazo bado zinaupungufu wa walimu wizara hiyo itahakikisha tatizo hilo linafanyiwa kazi ili kuleta mafanikio yaliyo bora kwa maendeleo ya jamii na  taifa kwa ujumla.

“Kuna baadhi ya viongozi wa kisisia wanadai eti wizara ya elimu imeshindwa kuajiri walimu hasa kwa upande wa Pemba nahao waliowaajiri hadi sasa ni walimu 8 nao wamepelekwa chokocho mimi nasema sikweli nakanusha kauli hiyo maana kuanzia mwezi wa kwanza, wapili na watatu kwa mikataba tofauti wizara yetu imeweza kutoa ajira za kutosha kwa wilaya zote za Pemba na kusambazwa maneo tofauti tofauti ambazo zinaonekana kweli kuna upungufu”

Aidha amesema kuwa wanaendelea kuifanyia kazi  kauli ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Ali Moh’d Shein ya kuwataka kuondoa tatizo lililojitokeza la upungufu wa walimu katika skuli mbali mbali  hivyo bado jitihada hizo  zinaendelea ili kuona kila skuli haileti malalamiko yoyote ya walimu.

Hatahivyo amesema kuongezeka kwa kasikubwa ya uandikishwaji wa wanafunzi na  Walimu kustaafu umepelekea kupungua  Walimu kwabaadhi maeneo hivyo kutoa nafasi kwa walimu wapya kuweza kuajiriwa.

“Tunaamini kuwa kuongezekwa kwakasikubwa ya uandikishwaji wa wanafuzi ambapo kwa mwaka huu umeongezeka mara dufu, na walimu kufikia muda wao wakustaafu kumeweza kuchangia hili pengo la upungufu wa walimu laki bado tumo mbioni kuweza kuliziba lisije kuleta athar yoyote”

Sambamba nahayo ameitaka jamii kutoskiliza kashfa hizo kwani hazina mashiko na hazina maslah kwao na badala yake waendelee kutoa mashirikiano yao yadhati pale ambapo panastahiki ili kuleta maendeleo makubwa ya kielimu hapa nchi.

Comments