Wakizungumza, baadhi ya
wanawake wa mkoa huo, walisema licha ya juhudi zinazochukuliwa na
wanaharakati wa kutetea haki za wanawake ili kukomesha vitendo hivyo,
bado baadhi ya watu wanaendelea kuwapiga wanawake.
Wakiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa
mpango kazi kuhusu vitendo vya udhalilishaji, walisema sababu ya
wanawake kupigwa zinatokana na ulevi wa waume zao na wivu wa mapenzi.
Akizungumza katika kikao hicho
kilichoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania
(TAMWA), mwanaharakati Zimba Khatib, alisema baadhi ya wanaume
wanaowapiga wake zao ni walevi kupindukia na wengine wamekithiri kwa
wivu.
Alisema wengi wa wanawake wanaopatwa na kadhia hiyo hawaripoti kesi hizo kwa kuhofia kuachwa.
Alisema ili kupunguza tatizo hilo jamii bado inahitaji elimu ya
kufahamu haki zao na kuchukua hatua pale vitendo hivyo vinavyowapata.
“Hali duni za maisha walizonazo wanawake pia zinachangia
kudhalilishwa kijinsia ikiwemo kupigwa na waume zao kutokana na
kuwategemea kwa kiasi kikubwa wanaume,” alisema.
Bahati Issa, Katibu mtandao wa ardhi wilaya ya kati, Mkoa wa Kusini
Unguja, alisema licha ya Mkoa huo kushamiri kwa vipigo lakini pia bado
watoto wanafanyiwa udhalilishaji.
Nae Meneja utetezi kutoka Tamwa Zanzibar, Hawra Shamte, alisema Tamwa
inaridhishwa na utendaji kazi wa wanaharakati hao wa kuibua changamoto
nyingi katika jamii.
chanzo: zanzibarleo.
Comments