Serikali yaivutia pumzi ZFA.


SERIKALI  ya Mapinduzi Zanzibar imesema kuwa inafuatilia kujua ukweli kama ZFA ilitumiwa barua ambayo, imetoa muongozo  wa umri kwa timu shiriki katika michuano ya CECAFA inayoendelea nchini Burundi.

Hatua hiyo ya Serikali imekuja  baada ya timu ya Taifa ya vIJANA Zanzibar  U-17 (Karume Boys) kuondolewa  kwenye michuao ya Chalenji ya Vijana kwa madai kuwa imepeleka vijana waliozidi umri.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo Omar Hassan (King), alisema kuwa pamoja na wao kufuatilia lakini inaitaka ZFA nayo kufuatilia njia za mawasiliano, ili kujua kwamba barua hiyo ilitumwa au la.

Alisema kuwa ikiwa ZFA itabainika walitumiwa barua hiyo na kusindwa kuitafsiri au kuisoma, ni muda wa chama hicho kuiangalia katiba yao na kujitathmini ili kuweza kuachia ngazi.

Alisema kuwa Serikali inafuatilia kuhakikisha kwamba ni kweli barua hiyo ilitumwa na wakiibaini kama kuna  uzembe umefanyika  Serikali itatoa maamuzi.

Hata  hivyo alisema kwamba kwa wakati huu, wametoa muda kwa chama hicho kufuatilia CECAFA na baadae kuja na majibu ambayo watayapeleka Serikalini ili waweze kuchukua hatua.

“Licha ya kuwa tunaiachia ZFA lakini tunafuatilia ila mpaka leo (jana) tulipowauliza  ZFA wanasema hawajatumiwa, sisi tunawapa muda waangalie njia za mawasiliano zilizotumika kutoka kwa Katibu mkuu wa CECAFA”, alisema.

Aidha alisema kuwa katika hilo Serikali itatoa majibu yake ndani ya mwezi mmoja ingawa alisema kuwa hawana uwezo wa  kuwawajibisha viongozi hao kutokana kuwa ni chama  huru na wao wana utaratibu wao  ila kwa katibu ambae yupo chini yao wakibaini watachukua hatua ambazo zitawaridhisha wote.

“Ikiwa tutabaini kwamba wametumiwa barua na wameshindwa kuzifuata kazi yetu tutawapa ushauri na wao wenyewe watajithmini ili waweze kuachia ngazi, lakini sidhani kwamba ndio sisi tumekuwa vilaza wa aina gani ili tuweze kushindwa kutafsiri vigezo na kanuni zlizotumwa katika barua hiyo”alisema.

Juzi Zanzibar ilitangazwa kutolewa kwenye mashindano hayo ambayo yanashirikisha vijana waliochini ya miaka 17 yanayofanyika nchini Rwanda kwa madai kuwa wameingiza wachezaji kinyume na muongozo uliotolewa na waandaaji wa mashindano hayp.

Katibu mkuu wa Wizara hiyo Omar Hassan (King) ametoa ufafanuzi huo mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu kadhia hiyo, ambayo imegusu nyoyo za Wanzabari wengi waliohuzunishwa na jambo hilo.

Alisema endapo itathibitika kuwa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) ndio wenye makosa mpaka hadi  Karume Boys kuondolewa katika Mashindano basi vyema wakawajibika kwa kujiuzulu.

Zanzibar iliondolewa katika Mashindano hayo na kupigwa faini kwa kosa la kuorodhesha wachezaji waliozaliwa kabla ya 01/01/2002 ambapo kanuni ya Mashindano hayo iliwataka wachezaji waliozaliwa tarehe hiyo, lakini  Zanzibar ilipeleka wachezaji 12 waliozaliwa 2001, jambo ambalo ZFA wamesema hawana taarifa kama wachezaji waliotakiwa ni wale waliozaliwa  2002.
 Zanzibarleo.

Comments