Mama Mwanamwema kuzindua chanjo ya saratani.

WIZARA ya Afya leo inatarajiwa kuzindua utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi hafla ambayo itafanyika Mwera wilaya ya Kati Unguja, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mke wa Rais,mama Mwanamwema Shein.

Chanjo hiyo itatolewa kwa wasichana waliofikisha umri wa miaka 14 Unguja na Pemba.

Kwa mujibu wa Ofisa wa Kitengo cha chanjo Wizara hiyo, Abdulhamid Ameir Saleh,lengo la kutolewa kwa chanjo hiyo ni kupunguza  saratani ya mlango wa kizazi kwa asilimia 80 katika kipindi cha miaka mitano.

Alisema,ili kupata kinga kamili,walengwa watahitaji kupata dozi mbili  ambapo ya pili  itatolewa miezi sita baada ya kupata ya dozi ya kwanza.

Alisema, chanjo hiyo ya HPV  inakinga maambukizi  ya virusi vinavyosababisha saratani ya mlango wa kizazi.

“Chanjo hii inaweza kupunguza matukio ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kiwango kibwa,” alisema.

Alisema, chanjo hiyo ni salama,imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Alisema, walengwa wote watasajiliwa na kupata kadi maalum inayothibitisha  kuwa amepata chanjo na kadi hiyo itaonyesha  tarehe ya kurudi kwa dozi ya pili na ambayo mlengwa amekamilisha  ratiba yake ya chanjo.

Chanjo ya HPV inawakinga mabinti dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi hapo baadaye  na ni salama ,haina madhara  na haimzuii binti kutopata watoto.

Alisema, walengwa wote watasajiliwa na kupata kadi maalum inayothibitisha  kuwa amepata chanjo na kadi hiyo itaonyesha  tarehe ya kurudi kwa dozi ya pili na ambayo mlengwa amekamilisha  ratiba yake ya chanjo.

Chanjo ya HPV inawakinga mabinti dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi hapo baadaye  na ni salama ,haina madhara  na haimzuii binti kutopata watoto.

chanzo: zanzibarleo.

Comments