
Mkuu
wa Wilaya Micheweni Mh. Salama Mbarouk Khatib amesema mapambano dhidi ya madawa
ya kulevya na ulawiti ndio kipao mbele
kwa mwaka huu ili kuweza kuwanusuru vijana, ambao ndio waathirika wakubwa wa matendo hayo.
Ameyasema
hayo huko katika skuli ya Elimu mbadala Wingwi Wilaya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati
akifungua mafunzo maalum kwa vijana wa wilayani humo yaliyo andaliwa na Jumuiya
ya Maendeleo ya Mikunguni ( MYDO) yenye lengo la kutoa hamasa kwa vijana
kujiunga na vyuo vya amali ili kuondokana na halingumu za kimaisha pamoja na
utegemezi wa ajira serekalini.
Amesema
wilaya yake imekuwa na idadi kubwa ya matendo maovu ikiwa nipamoja na ulawiti
na utumiaji wa madawa yakulevya ikilinganishwa na wilaya nyengine Pemba hali
ambayo imepelekea kundi kubwa la vijana ambao ndio tegemeo la Taifa kuathirika
kiafya nahata kisaikolojia.
Amesema
kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi nahata Polisi janmii watahakikisha
wanadhibiti matumizi, uuzaji na uingizaji wa madawa ya kulevya katika wilaya
hiyo.
"Vijana
wote wanajihusisha na utumiaji,
uuzaji na uingizaji wa madawa tunakula
nao sahani moja"Alisema Dc Salama.
Amefahamisha
kuwa nijuzi maeneo ya msasani wameweza kufanikiwa kukamata jumla ya madumu (28)
ambayo ni maroeko kwa ajili ya upikaji wa pompbe za kienyeji sambamba na
mitaimbo ya kupikia pombe hizo.
"Juzi
majira ya saa 4 usiku tulikamata madumu 12 na asubuhi yake tulifanikiwa
kukamata tena madumu 16".Alisema.
Aidha
amewataka wananchi wa wilaya hiyo kutoa mashirikiano yao yadhati kwa kutoa
taarifa pindi wanapoona vitendo hivyo vikiendelea huku akisema kuwa micheweni
bila madawa ya kulevya inawezekana.
Kwaupande
wake Mwenyekiti wa Mabaraza ya vijana Wilaya ya micheweni Pemba Nd. Ali
Suleiman Shaame amewataka vijana kuacha kukaa maskani na kufanya matendo yaliyokuwa
hayaleti maendeleo na badala yake kujiunga na mabaraza hayo ili kuweza kuunga
nguvu ya pamoja kwa kubuni miradi itakayo wasaidia katika maisha yao.
"Kijana
akiendelea kukaa maskani maranyingi hushawishika na kujiingiza katika vitendi
viovu, matuzi ya madawa ya kulevya, ulawiti na matendo mengine maovu, musingoje
kufikia huko njooni mujiunge na mbaraza haya tunufaike na fursa
zilizomo".Alisema.
Hatahivyo
amewataka vijana kutokaa tu ovyo
watafute kazi zakufanya zitakazo wasaidia kupata rizki zao za halali.
Comments