Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake Madema, Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir Ali, aliesema marehemu
ametambuliwa kwa jina la Omar Pauli Ziota (25) mkaazi wa Kibweni.
Alisema tukio hilo limetokea Aprili 4 mwaka huu saa 12:30 jioni ambapo kijana huyo alikuwa na wenzake wakiogelea.
Aidha alisema mwili wa marehemu umefikishwa hospitali ya Mnazimmoja
kwa ajili ya uchunguzi wa kidaktari na kukabidhiwa jamaa zake kwa
mazishi.
Wakati huo huo alisema Aprili 6 mwaka huu saa 8:40 mchana Mfenesini,
nyumba ya Khamis Ussi Machano (38) imeungua moto na kuunguza chumba
kimoja pamoja na vitu vyote vilivyomo chumbani humo.
Alisema vitu vilivyoungua vinakisiwa kuwa na thamani ya shilingi 1.7
milioni ambapo chanzo cha moto huo bado hakijajulikana huku upelelezi wa
shauri hilo bado unaendelea.
Chanzo: zanzibarleo.
Comments