
Akizungumza nje ya Mkutano wa kutathmini
Mpango kazi wa mwaka 2017 na kupanga Mpango kazi wa mwaka 2018/20 wa
kupambana na maradhi ya Malaria, Meneja huyo amesema Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo
wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kutokomeza ugonjwa huo lakini kuna
baadhi ya wananchi wanachangia kudumaza mafanikio hayo.
Amesema kitengo cha Malaria kimekuwa
kinachukuwa jitihada mbali mbali ikiwemo kupiga dawa majumbani na kugawa
vyandarua lakini baadhi ya watu wanakataa kutumia vyandarua kisheria na
badala yake wanavitumia kwa mahitaji yasiyostahiki na kusababisha
ugonjwa kutopungua katika makaazi yao.
Hata hivyo amesema kitengo cha kukabiliana
na malaria nchini kimeandaa utaratibu maaalumu wa kufatilia taarifa za
wagonjwa wa maradhi majumbani mwao ili kuweza kuwapatia matibabu
wangonjwa watakao bainika na Ugonjwa wa malaria kwa lengo la kuzuia
ugonjwa huo kuenea Nchini.
Awali akifungua Mkutano huo Waziri wa Afya
Zanzibar Hamad Rashid Muhammed amewataka wafanya kazi wa Wizara yaAfya
kuendelea kutumia vyema miradi ya maendeleo katika kutoa matibabu bora
kwa wagonjwa ili kupunguza matatizo yanayoikabili sekta ya afya ikiwemo
uhaba wa vitendelea kazi.
Aidha ametowa wito kwa wafanya kazi
kuhakikisha huduma na elimu ya kujikinga na Maradhi ya Malaria
inawafikia walengwa ili kuzuia maradhi hayo kurejea nchi na
kuisababishia hasara Serikali.
Nae Mkurugenzi wa Mradi wa Kumaliza Malaria
Tanzania Bara Waziri Nyoni amesema hali ya Malaria Tanzania bara
hairidhishi ambapo utafiti umeonesha kuwa Maradhi hayo yapo kwa asilimia
7.3.
Mkutano huo umeshirikisha wadau wa sekta ya
afya kutoka maeneo ya Zanzibar na nnje ya Zanzibar ili kufanya tathmini
ya maambukizi ya Ugonjwa huo pamoja na kuanda mikakati ya kuweza
kutokomeza Ugonjwa huo Nchini.
chanzo:Zanzibar 24.
Comments