Wazanzibar wametakiwa kuzitumia fursa za kibiashara kutangaza biashara wanazozalisha ili kupata wawekezaji.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja
mauzo na masoko wa shirika la magazeti ya serikali Tanzania TSN Januarus
Sebastian Maganga amesema tarehe 16 Murch TSN Imeandaa kongamano la
kibiashara Zanzibar kwa ajili ya kuibua fursa za kibiashara kwa
wafanyabiashara hasa wafanyabiashara wadogo ambao ni wajasiriamali ili
kuwasaidia katika kuonesha biashara zao kwani katika kongamano hilo
kutakuwa na wawekezaji.
Amesema TSN imekuwa mstari wa mbele katika
kusaidia wafanyabiashara katika mikoa mbalimbali Tanzania ikiwa na lengo
la kupambana na umaskini unaowakabili wananchi wenye kipato cha chini.
Maganga amesema katika kuelekea katika
uchumi wa Viwanda Tanzania serikali imekusudia kuwawezesha wananchi
kiuchumi kwa kutafuta wawekezaji kuwekeza nchni pamoja na kuwainua
wafanyabiashara biashara wadogo ili kwenda sambamba na lengo la Tanzania
kuondokana na umaskini.
Aidha ametoa wito kwa wajasiriamali
mbalimbali kushiriki pamoja na wananchi ili kuweza kutangaza biashara
zao wanazozalisha kwa kutumia rasilimali za asili.
Kongamano hilo linalotarajiwa kuhuzuriwa na
viongozi mbalimbali wa serikali ya Jamuhuri ya Muungano Tanzania pamoja
na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambalo linatarajiwa
kufunguliwa na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani.
Chanzo:Zanzibar24.
Comments