Serikali
mkoani Arusha kwa kushirikiana na wafanyabiashara, wametoa mikopo isiyo
na riba yenye thamani ya milioni 120 Kwa wajasiriamali wadogo wanawake
600 hatua ambayo itawasaidia kujikwamua kiuchumi.
Waziriwa
Sera, Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na Walemavu Jenister Muhagama,
akikabidhi mikopo hiyo jana jijini Arusha alisema serikali itaendelea
kuwakwamua wanawake kiuchumi, hii inatokana na asilimia kubwa ya utafiti
kuonyesha wanawake ndio wengi wanakabiliwa na changamoto zakutokuwa na
ajira .
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema kuwa huo ni mwendelezo
wakuwasidia wananchi wa hali ya chini wasiokopesheka na benki kutokana
na uwepo wamasharti magumu hivyo mkopo huo utawasaidia kujikwamua
kiuchumi.
Baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo Marrygoreth Leonard alisema itawainua kutoka hatua moja hadi nyinge na kujikwamua kiuchumi,
Wadau waliofanikisha mikopo hiyo akiwemo
Mfanyabiashara Willbard Chambulo, waliahidi kuendelea kuwasaidia
wanawake hao ili kupunguza umasikini katika kaya nyingi za wakazi wa
jiji la Arusha.
Mikopo
hiyo ni sehemu ya marejesho ya zaidi ya milioni mia tatu zilizotolewa
kwa waendelesha bodaboda katika mkoa wa Arusha ambazo wameshazirejesha.
Chanzo:Mpekuzi.
Comments