
Kauli hiyo ameitoa Mwenyekiti wa tume ya kurekebisha sheria Jaji Mshibe Bakari wakati akifungua mkutano wa wadau wa kujadili sheria ya msaada wa kisheria amesema lazima wadau wa sheria wajikubalishe kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kuondoa malalamiko kwa wananchi kwani imebaini wananchi wamekuwa wakiingia katika makosa kutoka na kushindwa kujua sheria na kushindwa kujitetea wanapofikishwa mahakamani hivyo wadau wa sheria wametakiwa kuwacha tama za fedha badala yake kufanya kazi kwa usawa.
Mshibe amesema wapo baadhi ya wananchi hususani wanyoge wamekuwa wanatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo kutokana na kushindwa kutoa ushahidi mahakamani hivyo uwemo wa mswaada huo wa kisheria utawasaidia katika kuwatetea wananchi ambao hawaweze kujitetea mbele ya mahakama.
chanzo:Zanzibar24.
Comments