Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mevlüt Çavuşoğlu ametoa indhari hiyo akizungumza na mwandishi wa habari wa Ujerumani juu ya uwezekano wa serikali ya Ankara kuwekewa vikwazo na Marekani, na kusema kuwa kamwe Uturuki haitonyamazia kimya hatua hiyo na badala yake itatoa jibu kali dhidi ya Washington.
Kadhalika Çavuşoğlu ameongeza kwamba, ni suala la kusikitisha kwamba baadhi ya nchi za Magharibi hadi sasa hazijafahamu ni namna gani zinatakiwa kuamiliana na nchi kama vile Uturuki.
Amesisitiza kwamba, Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya zinatakiwa zifahamu kwamba, Uturuki ni moja ya nchi washirika wakubwa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki ameelezea suala la kutolewa hukumu ya kifungo cha maisha kwa baadhi ya waandishi wa habari nchini humo na kusema kuwa, watu hao walihukumiwa adhabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kuwa wanachama wa kundi la Fethullah Gülen, mtuhumiwa mkuu wa jaribio la mapinduzi ya kijeshi ya tarehe 15 Julai 2016 au kwa kuwa na mahusiano na kundi la Kikurdi pa PKK.
Comments