
Akizugumza na Waandishi wa habari baada ya
Mazungumzo na wawakilishi wa Serikali ya China kuhusu kupambana na
Maradhi hayo, Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Muhammed amesema
wataungana bega kwa bega na serikali ya China kufanya utafiti utakao
wawezesha kukabiliana na maradhi hayo kwani yanaweza kuleta athari kubwa
kwa wananchi na kupoteza fedha za serikali pindipo yataenea katika
jamii.
Akizungumzia Mradi wa Maradhi
yasiyoambukizwaa unaofadhiliwa na Serikali ya China Mkuu wa kitengo cha
Maradhi hayo Dk.Fatma Kabole amesema mradi huo utajikita katika utoaji
wa dawa za kujikinga na maradhi hayo.
Amesema
Mradi huo pia umekusudia kumwaga dawa za kuuwa wadudu wanaosambaza
maradhi ya kichocho katika maeneo yote yenye kutuwama maji ikiwemo Mwera kwa Unguja na Kitongoji na Wingwi kwa Pemba na kutoa wito kwa wananchi kuwa na tahadhari ya kutumia maji yaliyotuama.
Aidha Waziri wa Afya nae ametoa wito kwa wafanyakazi wa wizara yake
kuendeleza ushirikiano mzuri kwa wadau wa maendeleo wanye malengo ya
kuanzisha miradi ya kutoa matibabu kwa wananchi ili waweze kunufaika na
huduma za matibabu zinazotolewa.
chanzo: Zanzibar24.
Comments