
Akizumgumza Mara baada ya kufunga Mkutano
wa kutathmini sekta ya elimu uliowakutanisha wadau mbalimbali wa
elimu nchni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mmanga Mjengo Mjawiri
amesema Wizara ya elimu imekubali kuyafanyia kazi matatizo yote
yanayoikumba sekta ya elimu ambayo yametajwa kuwa ndio chanzo cha
wanafunzi kutofanya vizuri katika mitihani yao.
Mmanga amesema atahakikisha mitaala ya
kufundishia inaenda sambamba na fani za wanafunzi watazozisomea
ambapo amefafanua kuwa kama mwanafunzi atakuwa anandoto za kuwa daktari
au mtaalamu wa kilimo basi mitaala hiyo iweze kumuwezesha kutimiza
malengo yao.
Aidha amesema kwa masomo ya sayansi wizara
itafanya kila njia kuhakikisha kila skuli inakuwa na maabara na vifaa
vya sayansi ili kuwawezesha kufanya vizuri katika masomo yao kwa njia ya
vitendo ambapo lengo kuu ni kuwa na elimu bora.
Hata hivyo amesema licha ya hayo pia
watahakikisha walimu wanaajiriwa wa kutosha ambao watakuwa na fani
zote na wenye sifa za kufundisha ili kutimiza ndoto za vijana kuweza
kufikia na kuwataka wanafunzi kuwa na bitii katika masomo yao kwani hivi
sasa serikali imejipanga kuinua sekta ya elimu kwa kiwango kikubwa ili
kuzalisha wasomi watakao kuwa wazalengo na kuweza kujakuitumikia nchi
yao.
chanzo: Zanzibar24.
Comments