
Sherine, ni mmoja wa waimbaji maarufu nchini humo pia ni jaji katika
kipindi cha mashindano ya waimbaji, The Voice- aliwaambia mashabiki wake
kuwa kunywa maji ya mto huo kunaweza kumpatia vijidudu “Kunywa Evian badala yake.” akatania.
Sherine, amehukumiwa na mahakama moja Cairo kwa kusambaza habari
zisizo za kweli. Chombo cha habari Misri, Ahram kimesema aliagizwa
kulipa paundi 5,000 za Misri.
Mashtaka dhidi ya Sherine yalifunguliwa mwezi Novemba, baada ya
kuonekana video mtandaoni ikimuonesha akiombwa kuimba wimbo uitwao
Mashrebtesh Men Nilha (umewahi kunywa maji ya mto Nile?).akajibu ”Nikinywa maji ya mto Nile nitapata kichocho”. Kichocho ni ugonjwa unaojitokeza maeneo ya vijijini nchini Misri.
Mbali na kesi hiyo mwanamuziki mwengine Shyma ilihukumiwa pia kwa kucheza video yenye kuonesha maadili mabovu
Maamuzi ya mahakama yaliyotolewa siku ya Jumanne inafanya idadi ya
wanamuziki kuhukumiwa kifungo kufikia watatu miezi ya hivi karibuni
Mwezi Desemba, Shaimaa Ahmed ajulikanaye kifupi Shyma alihukumiwa
kifungo cha miaka miwili baada ya kuonekana kwenye Video ya muziki akiwa
amevalia nguo za ndani huku akila ndizi kwa mbwembwe.
alikutwa na hatia ya kuweka video yenye maadili mabaya akahukumiwa
sambamba na muongozaji wa video hiyo.Baadae hukumu ilipunguzwa na kuwa
ya mwaka mmoja baada ya kukata rufaa.
chanzo: zanzibar24.
Comments