Msichana amuua mtoto wa miezi 7 kwa kumtumbukiza ndani ya ndoo Fuoni Unguja.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharib limempandisha Kizimba cha Mahakama ya Mkoa wa Vuga Shufaa Abdallah Suleiman mwenye umri wa miaka 24 Mkaazi wa Fuoni Mambo sasa kwakosa nla kuua kwa makusudi.

Imedaiwa na muendesha mashtaka Nyasi Ali mbele ya Hakimu Ali Ameir kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo tarehe 3 mwezi wa 10 mwaka jana saa 7 mchana huko Fuoni Mambo sasa Wilaya ya Magharib B.

Mtuhumiwa alimuua marehemu huyo kwa kwakiumtia katika ndoo iliyojaa maji, na kusababisha kifo chake.

Mtuhumiwa huyo hakutakiwa kujibu chochote kwakuwa kesi yake inataarishwa kusikilizwa Mahakama kuu na amepelekwa rumande hadi tarehe 13 mwezi ujao kesi yake itakapotajwa tena.

chanzo: zanzibar24.

Comments