Ahmed Aboul Gheit amesema hayo katika kikao cha dharura cha Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu waliokutana jana mjini Cairo Misri kwa shabaha ya kujadili uamuzi wa hivi karibuni wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusiana na Beitul-Muqaddas.
Riyadh al-Maliki, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Palestina amesema katika mkutano huo kwamba, uamuzi wa hivi karibuni wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Quds ni wa kijahili na wa kidhulma.
Tarehe 6 Disemba mwaka jana Rais Donald Trump wa Marekani alitangaza kuwa Washington inaitambua Quds (Jerusalem) kuwa ni mji mkuu wa Israel na kwamba itahamishia ubalozi wake katika mji huo kutoka Tel Aviv.
Uamuzi huo umepingwa na jamii ya kimataifa ukiwemo Umoja wa Ulaya.
Disemba 21 mwaka jana yaani siku chache baada ya uamuzi huo wa Trump, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipasisha azimio la kuunga mkono Quds.
Kwa mujibu wa azimio hilo, Umoja wa Mataifa ulitangaza kwamba, hautaitambua Beitul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
Mji wa Quds ulipo msikiti wa al-Aqswa kibla cha kwanza cha Waislamu ni sehemu isiyotenganishika na Palestina na ni moja ya maeneo matakatifu kwa Waislamu baada ya Makka na Madina.
Comments