takriban tani 1000 za mchanga zakamatwa Unguja.

Image result for UCHIMBAJI WA MCHANGA UNGUJAZaidi ya tani 1000 za mchanga zimekamatwa katika operation maalum iliyofanywa na idara ya misitu kituo cha polisi mwera   kwa kushirikiana na ofisi ya mkuu wa wilaya ya mgharibi A kufuatia  kupata taarifa za  kuchimbwa mchanga katika maeneo yasiyo ruhusiwa.

Akitoa taarifa hiyo mkuu wa kitengo cha maliasili zisizorejesheka Ngwali Makame haji amesema mchanga huo umekamatwa katika eneo la kianga na mwera uliochimbwa kutoka kambi ya jeshi welezo.

Aidha amesema mwezi Disemba mwaka jana  pia walikamata shehena 200 za mchanga katika maeneo ya Uzi  wilaya ya kusini  ambapo ulichimbwa katika mashamba ya kilimo na pembezoni mwa bahari.

Kutokana na hali hiyo amesema wameandaa kikao maalum ili kuondosha suala la uchimbaji wa mchanga kiholela kwa kupita kila wilaya ili  kuzungumza na wanaojishughulisha na shughuli hizo.


Sambamba na hayo amewataka wananchi na masheha kutoa taarifa ili kudhibiti uchimbaji wa mchanga katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Comments