

Akitoa wito huo Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakar Zuber wakati
akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya Maulidi iliyoandaliwa
na Kiwanda cha NIDA textile Mills|(T) ltd NAMERA GROUP OF INDUSTIES,
ambapo amewataka Waumini wa dini hiyo kusikiliza na kufuata kile
anachokisema Mtume.
“Nitoe wito kwa Waumini wa dini ya Kiislamu kufuata na
kusikiliza kile anachokisema Mtume kwa sababu Mtume amefundisha mambo
mbalimbali ambayo yana Maslaha kwa binadamu na ulimwengu wao,” Alisema Mufti Abubakar
Kwa upande wake Shekh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa
Salum ambaye alizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi pamoja na uongozi mzima
wa kiwanda cha NIDA amesema hafla hiyo inafanyika kila mwaka na kwamba
katika kufanya hivi kunasaidia amani ya nchi kuendelea kupatikana kwani
katika kuadhimisha Maulidi hayo wanafanya maombi hasa ya kuliombea
taifa.
Aidha amewashukuru uongozi wa NIDA pamoja na kuwapongeza kuweza
kuaanda Maulidi hayo kwani kwa kufanya hivyo wanawakumbusha waumini
pamoja na watu wa dini zote kutenda mambo mazuri kwa kutegemea ujira
mwema mbele ya allah (s.w)
Hafla hiyo imehudhuriwa na wageni mbalimbali Mgeni rasmi akiwa ni Mh.
Rais mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, alieambatana na
Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohammed Gharib Bilali na Viongozi
mbalimbali wa dini ya Kiislam .
chanzo: zanzibar24.
Comments