
Gavana wa Mombasa Hassan Joho, amezindua magari matano yenye mashine
na dawa kunyunyiziwa katika kaunti hiyo wakati ugonjwa unazidi
kuwatishia watu zaidi.
Chini ya miezi mitatu iliyopita kaunti ya Mombasa ilikuwa
ikikabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo watu kadhaa
walilazwa hospitalini na maeneo kadhaa ya mankuli kufungwa katika kaunti
hiyo.
Joho alithibitisha kuwa kumekuwa na visa 120 vya ugonjwa huo na visa
32 vilivyothibitiwa kati ya hivyo vimedai kuwa vile vya ugonjwa wa
chikungunya.
Kufuatia ugonjwa huo kusambazwa na mbu Gavana Joho amewashauri
wenyeji wa Mombasa kushirikiana kwa karibu na serikali ya kaunti kuondoa
mazingira salama kwa mbu.
CHANZO:BBC.
Comments