Wananchi watakiwa kutunza miundombinu ili kuleta maendeleo ya kiuchumi nchini.

Mkuu wa mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hassan Khatib Hassan amewataka wananchi wamkoa huo kujenga tabia za kuzitunza barabara na kuziweka katika hali ya mazingira ya usafi ili kuendelea kuimarisha shughuli za kiuchumi.

Mhe khatibu ameyasema hayo wakati akishiriki katika kazi za usafi wa pembezoni mwa barabara ya kitogani hadi paje kwa wanachama wa pressure group  meli nne taveta kinajijitolea kufanya kazi za usafi katika maeneo mbali mbali hapa nchini.

Amesema Serikali itaendelea na wajibu wake wa kuimarisha huduma muhimu za kijamii ikiwemo miundo mbinu ya barabara lakini jukumu la kuitunza litabaki kwa kila mwananchi hivyo ni vyema wakaunga mkono juhudi hizo ili ziendelee kuleta manufaa kwa jamii na taifa  kwa ujumla .

Amefahamisha kwamba uwekaji wa barabara katika hali ya usafi ni njia moja wapo ya kivutio cha wageni wanaoingia nchini jambo ambalo linasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza sekta ya utalii ambayo ni tegemeo kubwa katika kukuza uchumi.

Nao wanachama wa kikundi hicho wamesema wataendelea na juhudi zao za kujitolea katika  shughuli za kuweka usafi katika maeneo mbali mbali  mjini na vijjini.

Nae msimamizi wa njia wilaya ya kusini bwana Kussein Omar Hussein amewashukuru wana kikundi hao kwa jitihada zao walizozionyesha na kuwataka kuwa waangalifu wakati wanapofanya usafi pembezoni mwa barabara ili kuepukana kupasua mambomba ya maji yaliopita katika maeneo hayo.

chanzo: zanzibar24.

Comments