Waislamu wametakiwa
kuunganisha nguvu zao kwa pamoja kwa lengo la kukamilisha ujenzi wa mskiti mkuu
wa kidoti.
Akizungumza na Assalamu fm
katibu mkuu wa ijitimai Zanzibar Amir Hafidh Jabu amesema waislamu ni
vyema kushiriki kwa hali na mali ili kupeleka mbele harakati za dini ya
kiislamu.
Aidha amesema kina mama
wameonekana kujitokeza kwa wingi katika kuunga mkono ujenzi huo.
Kwa upande wao kina mama hao
wamesema wanafanya juhudi ili
kuhakikisha ujenzi unakamilika ikiwa ni pamoja na kujishughulisha katika kilimo ili kusaidia fedha kwa ajili ya
msikiti huo.
Mskiti mkuu wa kidoti wenye
uwezo wa kuchukua waumini 5100 unatarajiwa kuezekwa baada ya miezi
mitatu na utagharimu kiasi cha shilingi bilioni mbili na milioni mia nane hadi
kumalizika kwake.
Comments