Waislam nchi washauriwa kupenda kukisoma
kitabu kitakatifu cha Quran kwani ndio msingi wa maisha bora ya mwanandamu hapa duniani na kesho
akhera.
Ushauri huwo umwtolewa na Ustadh Ali
Nassor Abdallah wakati akifungua Madrasa ya Quran huko katika kijiji cha Uwaani
Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Amesema Quran ndio msingi mkuu wa maisha
hivyo kukisoma ni wajibu mkubwa kwa waislam na ndio ngao ya kuingilia peponi.
Amefahamisha kuwa kujengwa kwa madrasa katika
maeneo hayo kutaweza kuwaondolea usumbufu watoto wao na hata watuwazima kupata sehemu mzuri ya kukisoma kitabu cha
Allah na kuondokana na usumbufu wa kwenda masafa marefu hali iloyochangia
kukosa muda kabisa wa kujisomea.
Ameeleza kuwa inapaswa kuwashukuru wale
wote waliochangia ujenzi wa madrasa hiyo
kwani wameonesha moyo ya kujitolea hivyo nivyema kwa wakaazi wa eneo hilo
kuithamini na kuienzi ili iweze kuleta matunda mazuri kwa maslahi ya dunia na
akhera pia.
Aidha amewataka wafadhili walio jenga
madrasa hiyo kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja kwa kuwatafutia walimu ambao
wataleta msukumo mkubwa katika ufundishaji .
Akizungumza kwa niaba ya wanakijiji hao Ali Khamis Mbarouk amesema ujenzi wa madrasa hiyo utawesaidia kwa asi limia
kubwa watoto wao kupata elimu kwa ufanisi na kwawakati muafaka.
Ujenzi wa madarsa hiyo umefadhiliwa na
taasisi ya Istiqama Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Comments