Kufuatia jinai hiyo, Katibu Mkuu wa Harakati ya Aswaib Ahl al-Haq Bw.
Qais al-Khazali ametoa taarifa na kusema: "Kufuatia hatua ya helikopta
ya Marekani kudondosha mabomu katika eneo la al Baghdadi na kuuawa
Wairaqi kadhaa, haikubaliki tena kuendelea kubakia Jeshi la Marekani
nchini Iraq baada ya kushindwa kijeshi kundi la ISIS (Daesh).
Naye Ferdows al-Awadi, kutoka 'Muungano wa Utawala wa
Sheria' Iraq ambao unaongozwa na Nouri Al Maliki makamu wa rais wa Iraq,
pia ametoa tamko na kusema: "Mapatano baina ya Baghdad na Washington
ambapo yalitaka wanajeshi wa Marekani waondoke Iraq mwaka 2011 yana
faida gani katika hali ambayo bado kuna vituo vya kijeshi vya Marekani
katika maeneo yote ya Iraq na inaonekana kuwa vituo hivyo si vya muda.
Askari wa muungano wa Marekani unaodaiwa kupambana na ISIS wana vituo
kadhaa vya kijeshi nchini Iraq kwa ajili ya kile wanachodai kuwa eti ni
vita dhidi ya ugaidi.
Hii ni katika hali ambayo oparesheni za kijeshi nchini Iraq
zimepelekea kuuawa mamia ya raia wasio na hatia. Aidha wanajeshi wa Iraq
wamepoteza maisha katika hujuma za wanajeshi wa Marekani.
Utendaji kazi
huo mbovu wa wanajeshi wa Marekani ni dalili ya wazi kuwa wanajeshi hao
vamizi hawatoi msaada wowote wenye maana katika kutatua matatizo ya
kiusalama ya Iraq.
Matukio ya Iraq na mauaji ya kiholelea
yanayotekelezwa na wanajeshi wa Marekani ni ishara kuwa, Marekani
inataka kuchukua nafasi ya serikali ya kivuli katika nchi hiyo ya
Kiarabu.
Kwa kuzingatia nukta hizo,
swali linaloibuka ni hili kuwa, je wanajeshi wa Marekani wanataka nini
nchini Iraq? Je, inawezekana kutetea mauaji ya kiholela yanayotekelezwa
na wanajeshi wa Marekani jambo ambalo limekiuka mamlaka ya kujitawala na
uhuru wa Iraq?
Baadhi ya weledi wa mambo ya kisiasa wanaamini kuwa oparesheni za
kijeshi za Marekani nchini Iraq zinaashiria kurejea tena mezani ule
mpango wa awali wa watawala wa Marekani wa kuikoloni Iraq.
Aidha
Marekani inalenga kuibua serikali kibaraka katika nchi hiyo kubwa ya
Kiarabu yenye utajiri wa mafuta.
Baada ya kuangushwa utawala wa kiimla
wa Saddam mwaka 2003, Marekani ilimteua Jenerali Jay Montgomery Garner
kuwa liwali wa serikali ya mpito ya Iraq na baada ya hapo nafasi hiyo
ilichukuliwa na Paul Bremer.
Kufuatia kuwa macho viongozi wa kidini na
wananchi wa Iraq, njama hiyo ya Marekani ya kuteua watawala wa nchi hiyo
ilizimwa baada ya kufanyika uchaguzi na viongozi kuchaguliwa kwa kura
za wananchi.
Lakini pamoja na hayo, inaonekana Wamarekani hawakupoteza matumaini
na wangali wanaendeleza mbinu za kutekeleza njama hiyo. Moja ya hatua
zilizochukuliwa ni kujenga ubalozi mkubwa zaidi wa Marekani duniani
mjini Baghdad.
Ubalozi wa Marekani Baghdad una ukubwa wa ekari 104 na
inasemakana ukubwa wake ni sawa na wa Vatican. Ubalozi huo pia una
wafanyakazi karibu 2,000 na idadi hiyo inaendelea kuongezeka na
inatazamiwa kufika 17,000.
Swali linaliubuka hapa ni hili kuwa, je,
ubalozi huo mkubwa wa Marekani unafuatilia malengo gani na ni kwa nini
Wamarekani hawataki serikali ya Iraq ieneze mamlaka yake ya kujitawala
katika ardhi yote ya nchi hiyo?
Katika kipindi hiki cha utawala wa Donald Trump nchini Marekani,
serikali kivuli inayoongozwa na wanajeshi Wamarekani inaonekana kupata
nguvu Iraq.
Kumeshuhudiwa mara kadhaa uwepo wa wanajeshi wa Marekani
katika vituo kadhaa vya kijeshi Iraq na hata katika idara za kisaisa
nchini humo sambamba na kuvunjiwa heshima mamlaka na uhuru wa serikali
ya Baghdad.
Mfano wa wazi ni hujuma ya wanajeshi wa Marekani dhidi ya
msafara wa polisi mjini Ramadi, hujuma ambayo imetekelezwa katika fremu
ya kurejesha tena mpango wa George W Bush wa kuikoloni Iraq.
chanzo: parstoday.
Comments