Jumatatu ya jana Omer Dahab, mwakilishi
wa Sudan katika Umoja wa Mataifa, aliwasilisha mashitaka ya nchi yake
kwa Kairat Umarov, Mwenyekiti wa kiduru wa Baraza la Usalama la umoja
huo.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Dahab amelitaka baraza hilo
kushughulikia mashitaka hayo kama uthibitisho wa nchi yake kulalamikia
hatua ya Cairo juu ya eneo la Hala'ib.
Inafaa kuashiria kuwa, eneo la mpakani la Hala'ib lililopo ukingo
wa Bahari Nyekundu limekuwa likizozaniwa kwa muda mrefu kati ya Sudan na
Misri.
Tangu Sudan ilipopata uhuru mwaka 1955 imekuwa ikizozana na
jirani yake Misri juu ya umiliki wa maeneo ya Hala'ib na Shalateen.
Baadhi ya duru zinaamini kuwa, safari ya
hivi karibuni ya Rais Recep Tayyip Erdogan nchini Sudan imeshadidisha
vita vya maneno baina ya viongozi wa Khartoum na Cairo.
Comments