
Na Hamida Mohd Abdalla.
Vijana wa Jimbo
la Amani Shehia ya kwa Wazee wametakiwa kuwa kitu kimoja katika kuendeleza
maendeleo yanayopatikanwa ndani ya shehia
kutoka kwa viongoz wao.
Yameelezwa
hayo na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Shehia ya kwa wazee salmin Mussa Nahoda
huko ofisini amesema kuwa vijana wawe kitu kimoja bila kubaguana na itikadi za
chama, rangi, kabila na hata dini.
Aidha amewataka wazazi na walezi kuwa sio vyema
kuyatumia mabaraza ya vijana kwa itikadi ya kisiasa, kwani maendeleo wanayoyapata ni kwa ajili ya
wanachi wote wa jimbo na sio chama fulani.
Kwa upande
wake Katibu wa baraza hilo Harouna Ali amesema
ni vizuri kuzitumia fursa zinazotokea ndani ya shehia yao na kuendeleza
miradi inayotolewa ili kujikwamua na umasikini .
Hidaya Hassani
ni mmoja wapo aliejiunga ndani ya baraza hilo na kusema kuwa hawatoacha
kuwaunga mkono viongozi wao kwani
wamepata fursa nyingi kwa vijana wa shehia hio.
Comments