Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM)
Jumatatu ya jana lilitangaza kuwa, boti lililokuwa limewabeba wahajiri
150 lilizama katika pwani ya Libya baada ya kupata hitilafu ambapo
katika ajali hiyo wahajiri 64 walifariki dunia. Kwa mujibu wa ripoti
hiyo, watoto na wanawake kadhaa ni miongoni mwa wahanga wa ajali hiyo.
Kufuatia tukio hilo Tommaso Fabri, mkuu wa timu ya madaktari wasio na
mpaka nchini Italia amekosoa vikali siasa za uhajiri za serikali ya Roma
na nchi nyingine za Ulaya katika kujaribu kuwazuia wahajiri hao.
Jumapili iliyopita kuliripotiwa habari
ya kuzama maji wahajiri 25 katikka pwani ya Libya baada ya boti yao
kuzama wakiwa katika safari ya kuelekea Ulaya.
Kwa mujibu wa Shirika la
Kimataifa la Uhamiaji (IOM) zaidi ya wakimbizi elfu tatu waliaga dunia
mwaka jana wakijaribu kufika Ulaya kupitia Bahari ya Mediterania, vifo
ambavyo vingi vilitokea katika njia ya bahari kutoka Libya kuelekea
Italia.
Akthari ya wahajiri hao ni raia wa nchi za Kiafrika ambao
wanataraji kupata maisha mazuri na ajira huko barani Ulaya.
chanzo:parstoday.
Comments