Jeshi la Afghanistan: Kundi la kigaidi la Haqqani linahusika na mauaji mengi nchini.

Jeshi la Afghanistan: Kundi la kigaidi la Haqqani linahusika na mauaji mengi nchiniWizara ya Ulinzi nchini Afghanistan imetangaza kwamba, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Haqqani ambalo linaendesha harakati zake kwa jina la kundi la Daesh (ISIS), linahusika na mauaji mengi nchini humo.


Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema kuwa, kundi hilo la kigaidi linatekeleza mashambulizi yake kwa kutumia jina la kundi la Daesh kwa lengo la kuzipotosha fikra za walio wengi duniani. 

Imeeleza kwamba, kundi la Haqqani linafanya harakati hizo ili kuifanya serikali ya Pakistan iweze kusalimika na mashinikizo ya fikra za walio wengi na pia mashinikizo ya nchi nyingine.
Hii ni katika hali ambayo mashambulizi matatu ya umwagaji damu mkubwa hivi karibuni mjini Kabul na Jalalabad yalipelekea karibu watu 100 kuuawa ambapo kundi la Daesh lilitangaza kuhusika na hujuma hizo. 

Kundi la Haqqani ni tawi la operesheni la kundi la kigaidi la Taleban ambalo wanachama wake wamekuwa wakitekeleza mashambulizi mengi katika maeneo tofauti ya Afghanistan dhidi ya serikali na polisi ya nchi hiyo.
chanzo: parstoday.

Comments