Bahram Qassemi, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema
jinamizi la ugaidi haliwezi kutokomezwa pasina ushirikiano na jitihada
za pamoja za nchi za eneo na dunia nzima kwa ujumla.
Amesema, "kuukabili ugaidi kunahitaji ushirikiano wa dhati na juhudi
zisizo na kikomo za nchi za eneo hili la Mashariki ya Kati na dunia
nzima kwa ujumla."
Huku hayo yakirifiwa, idadi ya watu waliopoteza maisha katika
shambulizi hilo la jana imeongezeka na kupindukia 95, huku wengine zaidi
ya 200 wakijeruhiwa.
Hapo jana mripuko wa bomu la kutegwa ndani ya ambulensi ulitokea
karibu na ofisi za balozi za nchi kadhaa na majengo ya serikali katikati
ya Kabul, mji mkuu wa nchi hiyo.
Mtandao wa kigaidi wa Taliban umekiri kuhusika na shambulizi hilo,
wiki moja baada ya kutekeleza hujuma nyingine iliyoua watu zaidi ya 20
katika Hoteli ya Intercontinental mjini Kabul.
chanzo:parstoday.
Comments