Baraza la vijana laiomba ZMZ kuwaunga mkono katika kuleta maendeleo.

Baraza la Vijana Zanzibar limeiyomba Serikali kuwaunga mkono katika kuwasaidia upatikanaji wa malighafi ambazo watazitumia katika udhalishaji wa bidha zao za ujasiriamali.

Akizungumza Zanzibar24 Mwenyekiti wa baraza hilo Khamis Rashid Kheir amesema  vijana wamehamasika katika kufanya shughuli za ujasiriamali ambazo zitawasaidia katika kujikwamua na ukosefu wa ajira unaowakabili hivyo wameitaka serikali  kuwasaidia upatikanaji wa malighafi ili kuendelea na kazi zao.

Kwaupande wake Mjumbe wa baraza hilo Niki Abdi Singano  kutoka Shehia ya uzi amesema hali ya udhalishaji ipo vizuri ikiwemo sabuni,shampuu,losheni na vitu vyengine lakini  tatizo la upatikanaji wa malighafi linawarudisha nyuma.

chanzo:Zanzibar24.

Comments