

Vifaa hivyo ni miongoni mwa ahadi za Viongozi hao waliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi kuelekea katika mnasaba wa kutekeleza vyema ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2015/2020.

Balozi Seif alikabidhi vifaa hivyo wakati akimaliza ziara yake ya kutwa moja katika Jimbo la Chumbuni kwenye Mkutano wa Majumuisho uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Vifaa hivyo vinavyokadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi Milioni Tatu ni pamoja na Seti ya Jezi na Mipira Miwili kwa Timu Tano kwa niaba ya nyengine 14 zilizomo ndani ya Jimbo hilo.

Akizungumza na wanajimbo hao Balozi Seif ameupongeza mshikamano mkubwa unaoendelea kutawala ndani ya Jimbo la Chumbuni ambao unapunguza changamoto zinazowakabili watu wake.
Akitoa Taarifa katika Mkutano huo wa Majumuisho Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Ussi Salum Pondeza Maarufu Amjadi alisema Timu zote 14 za Soka kwenye Jimbo hilo tayari zimeshapata usajili wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar {ZFA}.
Amjadi alisema Uongozi wa Jimbo hilo utaendelea kuzihudumia Timu hizo katika masuala ya usajili, Vifaa pamoja na uwezeshaji ili ziweze kufanya vyema zinapoingia kwenye mashindano.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
24/1/2018.
chanzo:Zanzibar24
Comments