WENGER: MOURINHO PAMBANA NA HALI YAKO.

Jose Mourinho wa Man­chester United.
KOCHA wa Arsenal, Ar­sene Wenger amesema Jose Mourinho wa Man­chester United anatakiwa kupambana na hali yake na kuacha kulialia kuhusu ghar­ama za usajili uliofanywa na Manchester City.

Mara baada ya sare ya ma­bao 2-2 dhidi ya Burnley, Mourinho alisema kiasi cha pauni milioni 300 alichotumia kusajili tangu msimu uliopita hakitoshi kupambana na Man City kwa kuwa wao wametu­mia zaidi ya pauni milioni 360 kusajili.

Akizungumzia sual hilo, Wenger ambaye mara kad­haa amewahi kukwaruzana na Mourinho, amesema kupambana na timu zinazotumia gharama kubwa kusajili ni jambo la kawaida kwake na hata Mourinho anatakiwa kuzoea.
Ar­sene Wenger
“Nimekuwa katika hali hiyo kwa miaka 21, siwezi kuanza kula­lamika sasa kuhusu timu nyingine kusajili kwa gharama kubwa,” al­isema Wenger na kuongeza:
“Siku zote lazima kuwe na timu moja, wakati mwingine hadi nne ambazo zinakuwa ni tajiri kuliko sisi nimejifun­za kuishi katika mazingira hayo.

“Nafiriki jambo muhimu ni kupambana na mazingira yako kadiri unavyoweza, Manchester City ni matajiri zaidi yetu, hivyo ndivyo ilivyo kwa Chelsea na Manchester Unit­ed lakini bado ninaamini tunaweza kupambana na kufanikiwa.”

Comments