Lakini wameitaka kuziwekea vikwazo bidhaa zinazotoka nje ya nchi .
Wamesema kufanya hivyo kutasaidia kuimarisha viwanda vya ndani na kupata soko kubwa la bidhaa zinazozalishwa nchini.
Aidha wameitaka kuongeza
ushirikiano pamoja na kuzitaka serikali zote mbili zikae pamoja ili
kutatua baadhi ya changamoto za kisheria ili bidhaa zinazozalishwa
Zanzibar ziweze kuingia katika soko la Tanzania Bara na lile la Afrika
Mashariki.
Hayo yamesemwa leo
katika kikao cha Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha,
Biashara na Kilimo Yussuf Hassan Iddi wakati akisoma hutuba kuhusu
mswada wa sheria ya kuanzisha wakala wa maendeleo ya viwanda vidogo
vidogo na vya kati Zanzibar pamoja na kuwezesha ushajiishaji na
uendelezaji wa viwanda hivyo.
Kupitia Mwenyekiti huyo,
kamati imeipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuleta
mswaada huo katika wakati muafaka nchi ikiwa katika mageuzi kutoka
uchumi wa kutegemea kilimo kwenda uchumi wa viwanda.
Aidha alisema kuwa
uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo na vya kati nchini utawawezesha
wajasiriamali na wazalishaji wadogo wadogo kupiga hatua zaidi za
uzalishaji pamoja na kupata masoko ya ndani na nje kupitia usimamizi wa
wakala unaoanzishwa na sheria hiyo.
Alisema kwa kupitishwa
mswaada wa sheria hiyo, Zanzibar itaweza kupiga hatua kubwa na kuzalisha
ajira kwa vijana na kupunguza umasikini wa kipato kwa wananchi.
Alifahamisha kuwa ukuaji
wa uchumi wa nchi inategemea sekta ya viwanda kwa asilimia kubwa hivyo
mswaada huu unaweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wawekezaji na
wajasiliamali wa nje na wa ndani ili kuwekeza kwenye sekta ya viwanda .
Hata hivyo alisema
kupita kwa mswaada huu kutaifanya Zanzibar kufungua milango ya fursa za
kuinua uchumi na kupelekea pkuengezeka kwa pato la taifa (G.D.P).
Nae Waziri wa Biashara
na Viwanda na Masoko Mheshimiwa Balozi AmIna Salum Ali alisema mswaada
huu unaandika historia nyengine ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
katika kujenga maisha ya wananchi ili yawe mazuri katika kipato chao.
Aidha alisemamswaada
huo unaanzisha chombo ambacho ni wakala wa kusimamia maendeleo ya
viwanda vidogo vidogo ,vidogo na vya kati baada ya serikali kuona
changamoto mbali mbali zinazozikabili viwanda hivyo na kuondoa
mapungufu yanayojitokeza na kuwawezesha wazalishaji kuwa na mazingira
bora na kuzalishaji bidhaa.
Nao Wajumbe wa Baraza
hilo walisema mswaada huo utasaidia vijana wengi kupata ajira lakini
pia vijana hao waweke uaminifu katika uendeshaji wa kazi zao ili
kuimarisha viwanda hivyo.
Hata hivyo walisema nia
ya serikali ni nzuri lakini lazima ziondolewe changamoto mbali mbali
zinazowakabili ikiwemo mikopo ukosefu wa mikopo rafiki kwa
wafanyabiashara kutokana na kiwango kikubwa cha riba na soko la
uhakika la kuuzia bidhaa hizo pamoja na suala zima la kusimamia ubora wa
bidhaa hizo .
chanazo:zanzibar24.
Comments