Watupwa jela miaka 25 kwa kukutwa na mayai ya Mbuni yenye thamani zaidi ya milioni 42.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya  Serengeti imewahukumu kifungo cha miaka 25 washitakiwa wawili Marwa Matiko(32) na Julius Marwa (42) wakazi wa Tarime mjini, na gari lao kutaifishwa kwa kosa la kukutwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni.

Akitoa hukumu hiyo leo Ijumaa katika kesi ya uhujumu uchumi namba 128/2016 hakimu wa mahakama hiyo, Ismael  Ngaile amesema kila mshitakiwa atahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela na gari lao kutaifishwa liuzwe.


Mapema mwendesha mashitaka wa Jamhuri, Emmanuel Zumba ameiambia Mahakama kuwa, washitakiwa hao walikamatwa Desemba 7, 2016 wakiwa kwenye nyumba ya kulala wageni Serengeti wakiwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni ambayo waliyaficha ndani ya gari lao kinyume cha sheria.

Amesema washitakiwa wakidai kuwa walikuwa wanapeleka nchini Kenya kwa ajili ya kuuza kwa watu wanaotengeneza dawa ya ukimwi.

chanzo: zanzibar24.

Comments