
Akitoa maamuzi hayo
Mwenyekiti wa Mahakama hiyo Mohammed Subeit katika Mahakama ya Wilaya ya
Mwanakwerekwe kufuatia makosa hayo sambamba na kukosa sifa hatua
ambayo itapelekea baa hizo kutoendelea kufanyabiashara ya pombe kwa
mwaka 2018 hadi 2019.
Akizitaja baa hizo
zilizokosa vibali vya kuendelea na biashara kwa Wilaya ya Mjini na
Magharibi B ni Ras pub, Stone pub, na Valentine baa, Calfonia baa
amani, Jambo Migombani, Jose pub , In baa, Golden stoo, Habital baa ya
mitawi,titani na zebra kisauni amesema baa hizo zimekosa sifa kutokana
na mazingira yake na wamiliki wake hawafuati sheria za Vileo.
Aidha Subeit amewataka
wamiliki wa baa waliokosa vibali kama hawakuridhishwa na uwamuzi wa
mahakama ya wilaya waende mahakama kuu kwa ajili ya kukata rufaa.
Kwaupande wake Katibu wa
Kamati ya kupinga baa Zanzibar Abdalla Mnubi amesema amesikitishwa na
maamuzi ya mahakama na Wananchi hawakurizika kutokana baa walizozipinga
hazikufungiwa na hadi leo zinaleta usumbufu mkubwa katika makadhii
ya Wananchi.
Mnubi amesema licha ya
Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi kujitokeza kwa wingi katika kutoa
pingamizi zao mbele ya mahakama ya vileo lakini mahakama hiyo haikujali
na kuyatupilia mbali malalamiko yao juu ya baa hizo.
Aidha wametoa wito kwa
serikali kulisimamia suala la ongezeko la baa nchini ambazo huwaletea
usumbufu Wananchi hasa zilizopo karibu na maakazi pamoja na nyumba za
ibada zifungiwe ili kulinda maadili.
chanzo:Zanzibar24
Comments