Wanafunzi wapewa ushauri, suala la kufanya mapenzi.

Wanafunzi nchini  wameshauriwa   kuwacha  kujiingiza katika makundi maovu  ikiwemo  kufanya mapenzi  katika umri mdogo,mapenzi ya jinsia moja   ambayo  yatawaletea  athari na kukatisha ndoto zao katika kutafuta elimu.

Akizungumza  na Zanzibar24  baada ya utoaji wa elimu kwa wanafunzi wa skuli ya Mikindani  dole Mkuu wa dawati la kijinsi la Polisi madema Kassim Fadhil Abdalla amesema  nivyema wanafunzi   kuwachana na matendo  yasiyo  na  msingi   badala yake   kujikita katika   masoma ili kujitengezea matokeo mazuri, yatayowaletea matunda baadae.

Kassim amesema katika skuli hiyo zimeanza kuonekana ishara mbaya kwa wanafunzi  na tayari   kesi zimeanza kuripotiwa katika madawati ya kijinsi kuhusu matendo  maovu yanayofanyika katika skuli hiyo.
Kwaupande wao baadhi ya wanafunzi waliopata elimu hiyo Ruwaida Ahmada,Lailat Hamdani   wametoa ushauri   kwa wanafunzi wezao  kuwatayari kubadilika na  kutambua lengo walilolifata skuli na kuwacha kujiingiza katika  vitendo viovu ambavyo vitawazalilishaji.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na  taasisi mbalimbali  duniani  linatarajia  kuadhimisha Siku 16 za kupiga udhalilishaji kwa wanawake na watoto ifikapo tarehe 8  mwezi huu.
chanzo:Zanzibar24 

Comments