Wajumbe wa mikopo ya elimu watakiwa kusimamia vyema marejesho ya madeni.

Related image
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mmanga Mjengo Mjawiri amewataka wajumbe wa bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Zanzibar  kusimamia  vyema marejesho  ya madeni ya fedha walizokopeshwa wanafunzi wa elimu ya juu  ili kuipa uhai bodi wa kuendelea kuwa na uwezo wa kutoa fedha hizo kila mda utakapowadia.

Akizungumza wakati wa uzinduaji wa bodi mpya  ya awamu ya tatu ya mikopo   ya elimu ya juu huko mazizini amesema ili bodi hiyo iweze kujiendeleza lazima suala la mrejesho  wa fedha kusimamiwa  na kupewa kipaumbe kwa bidii kubwa hasa ukizingatia  wahitaji  wa mikopo bado wapo wengi  na wanahitaji kupatiwa fursa hiyo.

Amesema Zaidi ya Billion 35 zimetolewa  na Serikali  kwa njia ya mikopo  na hadi sasa fedha hizo zipo mikononi  mwa wanafunzi wanaoendelea na masomo  na wale waliohitimu elimu ya juu hazijarejeshwa ambapo  lisiposimamiwa na kufanyiwa kazi litaweza kuzorotesha maendeleo  na kuwakosesha wengine fursa hiyo kupewa kwa ajli ya kujiendeleza.

Aidha Mjengo ameitaka bodi hiyo kufanyakazi  kwa mujibu wa sheria kwa kuzingatia miongozo  iliyopo ili kuleta ufanisi ambapo ameahidi kuwa serikali haitakuwa nyuma katika ufuatiliaji wa mienendo ya utendaji kazi ya bodi hiyo.

Kwaupande wake Mwenyekiti Mstaafuu wa awamu ya Pili Kombo Hassan Juma amewataka watendaji hao kushirikiana na Wizara ya elimu katika kutafuta na kubuni mbinu mpya zitakazowezesha kupatikana kwa fedha zitakazoweza kukidhi mahitaji ya wanafunzi wa elimu ya juu na kuweza kujitegemea wenyewe.

Amesema Bodi bado inakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo Kasi ndogo ya makusanyo hivyo nivyema  kufanya jitihada za haraka kupambana ili kupata mafanikio  pamoja moja na kuandaa sera mahususi kwa wanafunzi wanaopata  fursa za  kwenda  kusoma nje ya nchi.

Aidha ameitaka bodi kuharakisha  marekejisho ya sheria ya bodi ya mikopo ili kuleta ufanisi  katika kazi za utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwani iliyopo inamapungufu.

chanzo:Zanzibar24

Comments