Viongozi wengine 7 wa upinzani akiwemo mbunge wakimbilia CCM.

Mwenyekiti wa Chama cha  Mapinduzi taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema CCM kimekuwa chama imara kinachoendelea kuwavutia watu wengi kila siku ikiwemo viongozi na wanachama kutoka vyama upinzani nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Desemba 18, 2017, kwenye Mkutano Mkuu wa 9 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao unafanyika mjini Dodoma na kusema kutokana na uimara wa CCM amepokea majina nane ya Madiwani wa vyama vya upinzani na Mbunge mmoja ambapo wanasubiri muda tu kutangazwa.


Nimepokea majina mengine ya viongozi wa upinzani ambao wanataka kurudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) wasaidizi wangu wameniambia yupo Mbunge mmoja anataka kurudi na ameniambia kuwa anataka kuja na madiwani saba kwenye jimbo lake, nasema hiki ni kimbunga na wataisoma namba kweli kweli.amesema Rais Magufuli.

Hata hivyo, Rais Magufuli amesema kuwa CCM wataendelea kupokea na kuwatangaza watu ambao wanahamia kwenye chama hicho na kudai kuwa lazima kwanza wajiridhishe ili wasije kupokea na watu wengine ambao hawana mpango mzuri kwa CCM.

Chanzo: zanzibar24.

Comments