Utafutaji wa mafuta na gesi asilia baharini katika visiwa vya unguja na pemba umekamilika.

mafuta
Mamlaka  ya Udhibiti wa Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar imesema itasimamia  kuhakikisha Mkandarasi  aliyekuwa anafanya kazi ya utafiti  wa gesi asilia baharini  anawalipa fidia wavuvi walioharibiwa nyavu zao wakati wa zoezi hilo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mamlaka hiyo Omar  Zuber amesema Mamlaka imekamilisha  zoezi la  utafutaji wa mafuta na gesi asilia  baharini katika  visiwa vya unguja na pemba lakini athari zilizojitokeza zitafanyiwa ufumbuzi  kwa kulipwa fidia wavuvi hao.

 Hata hivyo Omar amesema Zoezi hilo la utafiti  wa mafuta na gesi asilia  pia linatarajiwa  kufanyika  katika  nchi kavu  kwa baadhi  ya  maeneo na tayari baadhi ya vijiji vimesha orodheshwa kufanyika utafiti huo ikiwemo Jozani.
Amesema  zoezi hilo litaweza kuwagusa watu wengi  hasa  wakulima wenye mashamba   lakini Mamlaka imejipanga kikamilifu kuhakikisha  utafiti wake hautoathiri kwa kiwango kikubwa lakini kama itatokea matatizo yoyote iweze kukabiliana nayo kwa ulipaji wa fidia ili kuwaondolea wananchi walalamiko.
Idadi ya mistari iliyofanyiwa utafiti ndani ya kitalu cha pemba Zanzibar ni 62,ambapo ilikuwa na kilomita  2482 na kwa nje ya  kitalu ilikuwa mistari 4 na yenye kilomita 333.6.
CHANZO:Zanzibar24

Comments