
Akitoa ruhusa hiyo huko
katika Mahakama ya Wilaya Chwaka Mwenyekiti wa Mahakama hiyo Mohammed
Subeit amesema Bodi ya ukaguzi imefanya ukaguzi katika baa zote zilizopo
wilaya ya kati ikiwemo Chwaka, Uroa na Marumbi na imejiridhisha na
utendaji wa wenye mabaa.
Amesema vigezo
wanavyoviangalia katika ukaguzi wa baa nchini ni mazingira ya eneo la
biashara, ukataji wa lessen na vibali kwa mmiliki wa biashara hiyo,kama
eneo litakuwa na fujo au malalamiko ya wananchi sheria ya vileo
inaruhusu baa hiyo kufungiwa lakini kama vitakuwa hakuna tatizo lolote
hakutakuwa na pingamizi kwa mmiliki kunyimwa kibali cha kufanyia
biashara.
Hata hivyo amesema
wakati mahakama inaendelea na zoezi la kupokea maombi kwa wamiliki wa
baa Watendaji wa mahakama hiyo hawakupokea malalamiko wala tuhuma
zozote kutoka kwa wananchi wa Wilaya ya kati kama baa hizo zinaleta
usumbufu au matatizo yoyote.
Aidha Subeit ametoa
wito kwa wamiliki wa baa kufuata sheria zilizowekwa na mahakama ya
vileo na pindipo wataepuka kufuata maagizo waliyoambiwa mahakama haita
sita kuzifungia baa au kuwapokonya vibali vya biashara hiyo.
Jumla ya baa 21 zimeruhusiwa kuendelea kufanya biashara ya pombe kwa mwaka 2018 kutokana na kukidhi vigezo.
chanzo:Zanzibar24.
Comments