Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo ijumaa Desemba 8, 2017,
imeahirisha kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya
kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi na Mfanyabiashara, James
Rugemarila hadi Desemba 22, 2017, kutokana na upelelezi wa kesi hiyo
kutokamilika.
Harbinder Singh Sethi pamoja na Mfanyabiashara James Rugemarila, kwa
pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 yakiwemo ya kutakatisha fedha na
kuisababisha Serikali hasara ya zaidi ya Bilioni 3.
chanzo: zanzibar24.
Comments