Karibu watu 200,000 wakimbia moto wa nyika California.

Karibu watu 200,000 kwa sasa wamehamishwa kufuatia moto wa nyika huko California huku makundi ya uokozi Wazima moto 5,000 wamekuwa wakipambana na moto huo ambao umeharibu mamia ya nyumba kusini mwa jimbo la California.

Idadi ya watu waliohamishwa iliongezeka karibu mara nne siku ya Ijumaa baada ya moto wa tano kuzuka kaskazini mwa San Diego.

Wazima moto wakiondoa bidhaa kutoka kwenye nyumba za watu.
Firefighters remove a painting as they continue to extinguish fires in a home during the Kifo kimoja kimeripotiwa hadi sasa baada ya mwanamke mmoja kupatikana eneo lililokuwa limeteketea katika kaunti ya Ventura.

Hadi Alhamisi jioni, idara ya moto ya California ilisema kuwa moto ulilazimu kuhamishwa kwa watu 189,000.
Nyumba nyingi zilizo kwenye hatari ni za mamilioni ya dola
A huge plume of black smoke rises from a burning home on a hilltop beside one still standing in Bel Air, east of the 405 freeway on December 6, 2017 in Los Angeles, CaliforniaGavana wa California Jerry Brown ametangaza hali ya tahadhari eneo hilo.

Ikulu ya White House nayo inasema itatoa msaada wowote unaohitajika.

Upepo wenye joto wa Santa Ana wa jangwani umesababisha moto huo kuongezeka zaidi.
chanzo: zanzibar24.

Comments