HABARI ZA UHAMISHO JANUARI: PATA TETESI KUTOKA MAN UNITED, ARSENAL, CHELSEA, LIVERPOOL, BARCA, MADRID N.K.
MAN CITY WANAANDAA €56M KUMSAJILI BUSQUETS
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola yupo tayari kufanya mchakato wa kumsajili Sergio Busquets kutoka Barcelona, kwa mujibu wa Don Balon .
MAN UTD YAMWONGEZA KLUIVERT KWENYE ORODHA

Manchester United wamemwingiza Justin Kluivert kwenye orodha ya wachezaji wanaotaka kuwasajili dirisha la uhamisho wa Januari, kwa mujibu wa Yahoo Sport .
Kinda huyo wa miaka 18 mtoto wa gwiji la Kidachi Patrick amebakiwa na miezi 18 kwenye mkataba wake, lakini Thomas Lemar, Malcom na Christian Pulisic pia wameingia kwenye rada kwani Jose Mourinho anataka kusajili winga mpya kwenye kikosi chake.
ARSENAL YAPIGANA VIKUMBO NA UNITED KUMSAJILI RUGANI

Arsenal wameingia kwenye mbio za kumsajili beki wa Juventus Daniele Rugani, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Manchester United, the Sun limeripoti.
REAL YASAKA MNUNUZI WA RONALDO

Real Madrid ipo tayari kumuuza Cristiano Ronaldo ikiwa itatokea timu yenye dau nono Diario Gol .
Licha ya kuendelea kuongeza mataji kwenye klabu hiyo ya Hispania, kuna hisia ndani ya Santiago Bernabeu kuwa Mreno huyo nguvu zake zinaanza kufifia.
MAN UTD YAJIPANGA KUMSAJILI PULISIC

Manchester United imeingia kwenye kinyang'anyiro cha kumwania kiungo wa Borussia Dortmund Christian Pulisic, kwa mujibu wa Daily Mail .
LEMAR ANAPENDA KWENDA LIVERPOOL

Arsenal walishindwa kukamilisha dili la £90 milioni kwa ajili ya Lemar majira ya joto na inaaminika wanajipanga upya kumsajili winga huyo uhamisho wa Januari, Chelsea nao wakionyesha nia kumsajili.
SPURS YAMTENGEA DAU NONO SUAREZ

Tottenham wanaandaa dau nono kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez, kwa mujibu wa Don Balon .
Spurs wanaamini Barcelona watakuwa tayari kumuuza Suarez kwani wanalenga kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann, na miamba hao wa London wameshaanza mazungumzona wawakilishi wa mchezaji huyo.
Lakini mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool anasita kuondoka Camp Nou licha ya kuongezeka ushindani wa namba.
MAN UNITED YACHUANA NA REAL KUMPATA HAZARD

Manchester United wamejipanga kupigana vikumbo na Real Madrid kwa ajiliya saini ya Eden Hazard, kwa mujibu wa Sun .
Hazard na bosi wa United wamefanya kazi pamoja wakiwa Chelsea, na kufanikiwa kunyanyua taji la Ligi Kuu msimu wa 2014-15.
Na gazeti hilo limedai kuwa United watatoa dau la paundi milioni 90 kwa ajili ya mchezaji huyo msimu ujao.
PSG YAMFUATILIA DIARRA

Paris Saint-Germain wapo kwenye mazungumzo na mchezaji wa zamani wa Chelsea na Real Madrid Lassana Diarra, kwa mujibu wa SFR Sport .
Diarra kwa sasa anaichezea klabu ya Al Jazira ya Falme za Kiarabu, lakini anaweza kuruhusiwa kuondoka kwa uhamisho wa bure Januari.
NAPOLI YAMFUKUZIA KIUNGO WA CITY

Napoli itaanza upya jitihada za kumsajili kiungo wa Manchester City Oleksandr Zinchenko kwenye dirisha la uhamisho Januari, kwa mujibu wa TuttoMercatoWeb.
Zinchenko alijiunga na City mwaka 2016, lakini msimu uliopita alikuwa akitumika kwa mkopo PSV kabla ya kuivutia Napoli majira ya joto.
ATLETICO KUMUUZA GRIEZMANN KWA MAN UNITED

Atletico Madrid wapo tayari kumuuza Antoine Griezmann kwa Manchester United ili kuepuka kumuuza kwa Barcelona ambao ni wapinzani wao, kwa mujibu wa Metro .
MASCHERANO KUTIMKIA CHINA

Uhamisho wa Javier Mascherano kwenda Hebei China Fortune ni kama umekamilika baada ya Barcelona kukubali kumwachilia mchezaji huyo, kwa mujibu wa Marca .
Barcelona wanaweza kupata hadi milioni 10 kwa kumuuza beki huyo ambaye ameanza kukosa nafasi kikosi cha kwanza msimu huu.
ARSENAL INATAKA KUMSAJILI DAVID LUIZ

Arsenal wameandaa kitita cha £30milioni kwa ajili ya beki wa Chelsea David Luiz, kwa mujibu wa habari kutoka Daily Express .
Luiz ameichezea Blues mechi nane tu msimu huu Ligi Kuu Uingereza, baada ya kushindwa kumshawishi Antonio Conte.
Inafahamika kuwa mahusiano yao hayajapona vizuri, na Arsene Wenger sasa anavutiwa kuipata saini ya Mbrazili huyo.
Imeripotiwa kuwa Luiz ni shabaha ya Jose Mourinho na Manchester United, kadhalika Juventus na Real Madrid.
DE BRUYNE MBIONI KUSAINI MKATABA MPYA CITY

Kevin De Bruyne anakaribia kusaini mkataba mpya wa muda mrefu Manchester City, kwa mujibu wa BBC .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ameibukia kuwa mmoja wa viungo bora katika ulimwengu wa soka akiiwezesha timu ya Guardiola kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Uingereza kwa pengo la alama 11.
ARTETA APANGWA KUWA MRITHI WA WENGER

Mikel Arteta ndiye anayeweza kupewa mikoba ya Arsenal kumrithi Arsene Wenger, kwa mujibu wa Daily Telegraph .
The former Spain international is currently working at Manchester City under Pep Guardiola, but is held in high regard by the Gunners.
Wenger's current contract expires in 2019, and Arsenal are working up a shortlist of replacements, with Arteta near the top of the list
Mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Hispania kwa sasa anafanya kazi Manchester City chini ya Pep Guardiola, lakini anapewa nafasi kubwa na Gunners.
Mkataba wa Wenger unafikia mwisho 2019 na Arsenal wameanza kuangalia makocha wanaoweza kuwa mbadala wake, Arteta akiwa wa kwanza kwenye orodha.
DORTMUND WANANAMTAKA MKHITARYAN WAO

Borussia Dortmund wanaendelea kuonyesha nia ya kumrejesha mshambuliaji wa Manchester United Henrikh Mkhitaryan kwenye klabu yao, kwa mujibu wa The Independent .
Mkhitaryan aliondoka Dortmund kutua Old Trafford majira ya joto 2016, lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Armenia ameshindwa kuleta ushawishi chini ya Jose Mourinho.
Bosi wa United hajakataa uwezekano wa kuuza wachezaji Januari, na kufuatia habari zilizojiri anaweza kumruhusu Mkhitaryan kurejea Bundesliga na kumruhusu Mourinho kumsajili Julian Weigl.
MAN UTD YATENGA £60M KUMSAJILI SANDRO

Manchester United wanajipanga kutoa kitita cha paundi milioni 60 kwa ajili ya beki wa Juventus Alex Sandro uhamisho wa Januari, kwa mujibu wa Daily Mirror .
Bosi wa United amekuwa akivutiwa na kazi ya Mbrazili huyo mara kadhaa kwani anataka kuimarisha zaidi safu yake ya mabeki Old Trafford.
ARSENAL KULIPA €48M KUMSAJILI LOZANO

Arsenal wapo tayari kutoa €48 milioni kwa ajili ya nyota wa PSV Hirving Lozano, kwa mujibu wa habari kutoka Mexico.
Lozano anacheza Eredivisie msimu wake wa kwanza na ameshafunga magoli 10 na kutoa pasi sita za magoli katika mechi 15 tu msimu huu, akizivutia Gunners na Everton.
DORTMUND YAKARIBIA KUMPATA ROMERO

Borussia Dortmund inakaribia kumsajili Maximiliano Romero kutoka Velez Sarsfield, Bild limeripoti.
Mshambuliaji huyo, 18, anaweza kugharimu takribani €12 milioni, na Dortmund wanaamini anaamini atakuwa mrithi sahihi kwa Pierre-Emerick Aubameyang.
WEST HAM WAMTENGEA DAU ARTER

West Ham wanataka kumsajili Harry Arter kutoka Bournemouth, kwa mujibu wa The Sun .
Bosi wa Wagonga nyundo David Moyes anataka kuimarisha safu yake ya kiungo na anaamini kuwa Arter, ambaye hajapata nafasi kikosi cha kwanza msimu huu ni suluhisho sahihi.
BARCA YAKARIBIA KUMSAJILI KINDA WA ZAMANI WA CITY

Barcelona wanakaribia kumsajili kinda nyota wa zamani wa Manchester City Jose Angel Pozo, kwa mujibu wa Onda Cero .
Comments