
Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Makomero na Mwabakima vilivyoko wilayani humo katika hafla ya uzinduzi wa sheria hizo, alisema mazingira ya wilaya hiyo sasa yatakuwa bora kwa kuwa vitendo vya uharibifu vitadhibitiwa.
Alisema kukithiri kwa vitendo vya ukataji miti ovyo, kuchoma moto, kuharibu vyanzo vya maji na kujisaidia ovyo kulichangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa sheria zinazoweza kuwabana wahusika katika vijiji na mamlaka ya mji.
Mwanri alifafanua kwa kuwa sheria hizo zimependekezwa na wananchi wenyewe, hata zilipofika ofisini kwake hakusita, alizipitia na kusaini moja kwa moja, hivyo akawataka kuzitekeleza ipasavyo ili kujiletea maendeleo.
Aliwataka wenyeviti wa vijiji, watendaji na madiwani kuzisambaza na kuhamasisha wananchi wao kuzisoma na kuzielewa ili watambue hatua za kisheria zitakazowakabili punde watakapokwenda kinyume nazo.
Akizungumza kwa niaba ya wanakijiji, Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Makomero, Zefania Kilo alimpongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuzindua sheria hizo na kwa kuanzia alisema atahakikisha kila kaya inakuwa na choo bora na kupanda miti isiyopungua mitano.
chanzo:Habarileo
Comments